Aika Swai, New York, USA
"Sisi tunaoishi nje tunawaomba kina baba na mama, kaka na dada mumpe kura zenu
Kikwete na Karume. Maisha bora kwa kila mtanzania."
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Jakaya Kikwete, ndiye atakayepeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kampeni za uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika makala hii, Mwandishi Wetu EPSON LUHWAGO anachambua kwa undani uwezo wa mgombea huyo katika medani ya uongozi kitaifa na kimataifa.
Wamiminika barabarani kutaka awasalimu Wengi warejea CCM Na Epson Luhwago, Kilwa Masoko KUTOKANA na mvuto alionao mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Jakaya Kikwete, wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kibiti jana walizuia msafara wake kwa nguvu na kumsomea risala kwamba vijana wote wanaunga mkono CCM na watawapigia kura wagombea wake.
MAENEO mbalimbali ya mkoa wa Mtwara aliyopita mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete, jana yalizizima kufuatia kujitokeza watu kwa wingi kumsikiliza katika mikutano yake ya kampeni.