Kikwete hakumshambulia Banduka
Guestbook
Tanzania, is a country on the east coast of east Africa.
 
JakayaKikwete.com
 »  Home  »  Habari Mpya  »  Kikwete hakumshambulia Banduka
Kikwete hakumshambulia Banduka
By Ikulu Press | Published  08/4/2007 | Habari Mpya | Rating:
Katika gazeti lako la leo  4/8/2007, ukurasa wa mbele kuna habari yenye kichwa  Kikwete amshambulia Banduka.
 
Ofisi ya Rais Ikulu, inapenda kutoa ufafanuzi  kuhusu habari hiyo,  lakini pia Ofisi ya Rais inaamini kwamba mwandishi wa habari aliyekuwapo wakati Mkuu wa Mkoa akitoa taarifa ya mkoa kwa Rais ameiandika habari hiyo out of propotion.
 
Ni kweli kwamba mkuu huyo wa mkoa katika taarifa yake alimweleza Rais  kuhusu matatizo ya  uhaba wa ardhi unaowakabili wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro,  na  pia  akaeleza pia juhudi mbalimbali zinazofanywa na  uongozi wa mkoa kukabiliana na  tatizo hilo.
 
Baada ya kuuliza maswali kadhaa ya kutaka kupata taarifa za kina juu ya tatizo hilo na juhudi hizo za mkoa, ndipo  Rais alipoushauri  na  kuutaka uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kufanya mazungumzo na viongozi wenzao wa mikoa mingine na kuangalia uwezekano wa kupata maeneo ya kuwapeleka wananchi hao.
 
Alisisitiza suala la maandalizi kwa maana ya kufanya mazungumzo na viongozi wa maeneo husika kabla ya kutoa matamshi ya kuwapa matumaini wananchi kwamba watapelekwa eneo fulani.
 
Ni katika msisitizo huo wa kuwataka viongozi kufanya maandalizi mazuri kwa kufanya majadiliano kati yao , viongozi wenzao na wananchi walengwa ndipo alipotoa mfano wa matamshi ambayo huko nyuma yaliwahi kutolewa  Ndugu  Banduka, wakati huo akiwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani kwamba  wananchi wapatao 46,000 wangehamia   mkoani Pwani  ili hali hakukuwa na maandalizi yoyote yaliyofanyika.
 
Rais aliutoa mfano huo wa  Ndugu. Banduka kwa nia njema kabisa, na hata namna alivyoueleza mfano huo ulikuwa katika lugha   nyepesi ambayo haikuonyesha kama kulikwa na dalili au hata chembe  ya kumshambulia Ndugu. Banduka Kama  Mwandishi alivyoeleza.
 
Ofisi ya Rais imesikitishwa  sana na taarifa  hiyo kwa namna ilivyoandikwa na hasa alivyoifanya kuwa habari kubwa na kichwa cha habari  kinachoweza kusababisha chuki katika jamii bila sababu zozote na msingi.
How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent

Verification:
Enter the security code shown below:
img


Add comment
Comments