Taarifa ya Ziara ya Rais Lindi - Ruangwa
Guestbook
Tanzania, is a country on the east coast of east Africa.
 
JakayaKikwete.com
 »  Home  »  Habari Mpya  »  Taarifa ya Ziara ya Rais Lindi - Ruangwa
Taarifa ya Ziara ya Rais Lindi - Ruangwa
By Premi Kibanga | Published  11/19/2007 | Habari Mpya | Rating:
 

Serikali imekikopesha Chama cha Ushirika cha Ilulu shilingi milioni 769 kwa ajili ya ununuzi wa Korosho katika Mkoa wa Lindi.

Rais Jakaya Kikwete amewaambia wananchi wa Ruangwa leo asubuhi mara baada ya kuwasili wilayani humo kuendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Lindi.

Mara baada ya kufika mkoani Lindi kuanza ziara Jumanne wiki hii na kuelezwa matatizo ya ununuzi wa zao hilo kubwa la biashara mkoani Lindi, Rais aliwaahidi wananchi kuwa atawatatulia tatizo la mikopo kabla hajamaliza ziara yake kwa kuzungumza na Waziri wa Fedha ili pesa zaidi zitolewe kwa ajili ya ununuzi wa Korosho.

“Nimeongea na Waziri wa Fedha kuhusu tatizo lenu hilo na ameniahidi kuanza kutoa pesa hizo wiki hii ili muondokane na adha mnayoipata” Rais amesema.

Mapema Chama cha Ushirika kiliomba kukopeshwa shilingi bilioni 1.5 lakini walipewa mil.731 ambazo mbali na kununua korosho pia zimetumika kununua vitabu, magunia na usafiri hivyo hazikutosheleza mahitaji ya ununuzi na ndipo wananchi wakatoa kilio chao kwa Rais na amewasaidia kutatua tatizo hilo.

Hata hivyo pesa hizi zinaonekana kuwa bado hazitatosheleza mahitaji yao hivyo Serikali imeahidi kuwa kutoka sasa wataendelea kukopeshwa ili azma ya Serikali ya kuwasaidia wakulima kujikwamua na kujiongezea kipato hatimaye itimie na mkulima afaidike pia kwa kuuza kilo moja kwa shilingi 610 na hatimaye bei hiyo iendelee kukua na kuimarika.

Rais Kikwete ambaye yuko mkoani Lindi na kufuatilia utekelezaji wa ahadi za CCM kwa wananchi, Rais Kikwete pia amefungua rasmi daraja la Mbwemkuru juu, linalounganisha wilaya za Ruangwa na Kilwa lililogharimu Halmashauri za Wilaya hizo na Serikali Kuu milioni 166. Kabla ya kujengwa kwa daraja hilo, wananchi wa wilaya hizo walikuwa wametengwa na mawasiliano kati yao yalikuwa magumu..

Daraja hili litawafaidisha wasafiri ambao hulazimika kupita Lindi wanaposafiri kwenda Dar-es-salaam na pia wakulima ambapo sasa watasafirisha mazao yao kwa wakati.

Rais amesema anafanya taratibu kuiingiza barabara inayopita katika daraja hilo kwenye ngazi ya mkoa kutoka wilayani ili ifanyiwe mpango wa pesa na hatimaye kufanyiwa marekebisho makubwa ipate kupitika wakati wote

Rais pia amezindua kituo cha afya Nanjilinji, nayo ni hatua kubwa za Serikali katika kupunguzia wananchi adha ya kusafiri zaidi ya kilometa 5 kutafuta huduma ya afya. Katika vituo hivyo vya afya vinavyotarajiwa kujengwa kote nchini, huduma za ukunga pia zitatiliwa mkazo ili kuwaondolea adha wazazi na pia kupunguza idadi ya vifo vya akina mama na watoto.

“Moja ya shabaha zetu kubwa ni kuendeleza huduma za afya nchini, tunataka kila mwananchi apate huduma za afya zilizo bora, hivyo mwakani tunaanza mpango wa kuwa na zahanati kila kijiji na kila makao makuu ya kata kuwe na kituo cha afya” Rais amesema na kuwakumbusha wananchi kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa Ukimwi ambao hauna dawa.

Mara baada ya kuingia madarakani Serikali imeahidi kuleta maisha bora kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za afya, elimu, miundo mbinu na kuinua hali ya kipato cha wananchi.

Tayari hatua kubwa imeshafikiwa katika ujenzi wa shule katika kila kata nchini kote na tayari Serikali imeshaweka mipango ya kuanza ujenzi wa vituo vya afya na zahanati karibu na wananchi wake.

Katika kuhimiza elimu bora na kwa kila mwananchi pale alipo, Rais Kikwete pia amefungua majengo matatu ya maabara ya shule ya sekondari ya Mbekenyera wilayani Kilwa na baadaye kuweka jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za National Housing Cooperation (NHC) huko Kilimahewa Ruangwa kabla ya kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara.

Rais Kikwete amewahimiza wananchi kujenga shule za masomo ya Sayansi chini ya Education II Project. Mradi huu umejumuisha ujenzi wa maabara 3, hosteli ya kulala wasichana wapatao 20. Amewataka wananchi kujenga maabara kwenye shule zote za sekondari ili wapatikane wataalamu wa kuleta maendeleo nchini.

Gharama ya ujenzi ni shilingi milioni 200 ambazo zimetolewa na African Development Fund (ADF) ikiwa ni mkopo kwa Serikali ya Tanzania.

Rais ameahidi kuchangia shs. Mil. 10 kwa ajili ya kusaidia ukarabati wa mabweni manne (4) ya wasichana na kuhimiza wazazi pia kujenga mabweni kwa ajili ya wavulana ili watoto wengi waende shule.

Mkoa wa Lindi una matatizo makubwa ya watoto wa kike kupata mimba wangali shuleni.

Rais Kikwete kesho ataendelea na ziara yake Lindi vijijini.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent

Verification:
Enter the security code shown below:
img


Add comment
Comments