Articles by this Author
»
Serikali kunusuru mahindi Ruvuma - Lowassa
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amesema serikali inakusudia kuyanusuru mahindi ambayo yamekosa soko katika mkoa wa Ruvuma kwa kuyanunua kupitia Kitengo cha Akiba ya Chakula cha Taifa (SGR).
»
Lowassa aahidi umeme vijijini na amfariji muathirika wa tetemeko
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amesema leo (Alhamisi Agosti 23, 2007) serikali imetenga zaidi ya Sh. Bilioni 10 kuanzia mwaka huu kwa ajili ya miradi ya kusambaza umeme vijijini.
»
Lowassa kufunga kambi ya kimataifa ya vijana Manyoni Jumapili hii
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa anatembelea Wilaya ya Manyoni mkoani Singida kesho (Jumapili Agosti 12, 2007) kufunga rasmi kambi ya kimataifa ya vijana ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Vijana (International Youth Day).
»
Waziri Mkuu Lowassa ashiriki bonanza la michezo la ofisi yake leo asubuhi mjini Dodoma
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa alitembea kwa mguu na baadaye kupiga mpira uliotikisa wavu wakati akizindua na kushiriki mjini Dodoma leo (Jumamosi Agosti 11, 2007) asubuhi katika Bonanza la Michezo la wafanyakazi wa Ofisi yake.
»
Wakurugenzi zaidi wa mamlaka za Serikali za Mitaa wahamishwa.
MAJINA zaidi ya Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa waliohamishwa kutokana na kuanzishwa Halmashauri za Wilaya mpya na kuteuliwa kwa Wakurugenzi wapya hivi karibuni yatajwa.
»
Rais Kikwete amteua Prof. Wangwe kuwa mwenyekiti kituo cha Elimu Kibaha.
RAIS Jakaya Kikwete amemteua Profesa Samwel Wangwe wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Elimu Kibaha.
»
Lowassa ateua wakurugenzi wapya wa Wilaya
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa amewateua Wakurugenzi wapya wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuwadilisha wengine vituo vyao vya kazi.
»
Lowassa awashushua Wapinzani
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amesema mipango mizuri iliyowasilishwa Bungeni yenye nia ya kuendeleza utalii nchini ni utekelezaji wa sera za CCM na siyo mapendekezo ya wanasiasa wa upinzani.
»
Mzabuni wa vitambulisho vya Taifa hajateuliwa
SERIKALI bado haijateua mzabuni wa kutengeneza vitambulisho vya taifa nchini na kwamba kazi hiyo itasimamiwa na taasisi ya vitambulisho vya taifa iliyoanzishwa nchini.
»
Lowassa kuwauliza wakuu watatu wa mikoa kwanini timu za mikao yao hazikuhudhuria mashindao ya raidha.
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amesema atawauliza Wakuu wa Mikoa ya Kigoma, Lindi na Mtwara kwa nini timu za mikoa yao hazikufika kwenye mashindano ya kitaifa ya riadha aliyoyafungua mjini Dodoma leo (Ijumaa Juni 29, 2007).